Everton – Greensports Site: Habari za michezo na burudani Tanzania na Ulimwenguni. https://www.greensports.co.tz Michezo na burudani ni zaidi ya ajira Tue, 16 Apr 2024 07:00:56 +0000 en-GB hourly 1 https://wordpress.org/?v=6.5.5 https://www.greensports.co.tz/wp-content/uploads/2021/09/cropped-WhatsApp-Image-2021-09-02-at-13.12.19-1-32x32.jpeg Everton – Greensports Site: Habari za michezo na burudani Tanzania na Ulimwenguni. https://www.greensports.co.tz 32 32 Everton wakomalia pointi 6 walizopokwa https://www.greensports.co.tz/2024/04/16/everton-wakomalia-pointi-6-walizopokwa/ https://www.greensports.co.tz/2024/04/16/everton-wakomalia-pointi-6-walizopokwa/#respond Tue, 16 Apr 2024 07:00:55 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=10612

London, England
Rufaa ya Everton kupinga kupokwa pointi kwa kosa la kwenda kinyume na kanuni za Ligi Kuu England za matumizi ya fedha, itasiklizwa haraka na uamuzi kutolewa kabla ya kumalizika kwa msimu wa ligi.
Awali Everton ilipokwa pointi 10 na baadaye adhabu kubadilishwa na kuwa pointi sita baada ya kukata rufaa Februari mwaka huu kwa kosa ambalo wanadaiwa kulifanya kwa miaka mitatu hadi kufikia msimu wa 2021-2022.
Taarifa ya wasimamizi wa Ligi Kuu England ilieleza kuwa klabu ya Everton ilikata rufaa Jumatatu (jana) na rufaa hiyo itasikilizwa haraka.
Everton inayonolewa na kocha Sean Dyche kwa sasa inashika nafasi ya 16 katika msimamo wa Ligi Kuu England ikiwa na pointi mbili zaidi ambazo zinaitoa kwenye hofu ya janga la kushuka daraja.
Kanuni ambayo Everton inadaiwa kuivunja inahusu faida endelevu ambapo klabu zinaruhusiwa kupoteza au kupata hasara isiyozidi Pauni 105 milioni kwa kipindi cha miaka mitatu lakini Everton inadaiwa kuzidisha kiasi hicho kwa Pauni 16.6 milioni kwa kipindi cha miaka mitatu hadi msimu wa 2022-2023.
Hata hivyo kuna hofu kwamba suala hilo huenda likachukua muda kufikia hitimisho hadi baada ya msimu huu wa Ligi Kuu England.
Mechi za mwisho za Ligi Kuu England zinatarajia kuchezwa Mei 19 na tayari wajumbe wa bodi watakaosikiliza rufaa hiyo wameshatangazwa.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/04/16/everton-wakomalia-pointi-6-walizopokwa/feed/ 0
Everton yapunguziwa adhabu EPL https://www.greensports.co.tz/2024/02/26/everton-yapunguziwa-adhabu-epl/ https://www.greensports.co.tz/2024/02/26/everton-yapunguziwa-adhabu-epl/#respond Mon, 26 Feb 2024 18:51:36 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=9895

London, England
Adhabu iliyopewa klabu ya Everton ya kupokwa pointi katika Ligi Kuu England (EPL) kwa kosa la kwenda kinyume na kanuni ya matumizi ya fedha, imepunguzwa kutoka pointi 10 za awali hadi sita.
Hatua hiyo imekuja baada ya Everton kuikatia rufaa adhabu ya awali ya kupokwa pointi 10 iliyotolewa Novemba mwaka jana baada ya klabu hiyo kudaiwa kukiuka kanuni inayohusu faida na ustawi wa klabu au PSR kwa kipindi cha miaka mitatu hadi msimu wa 2021-22.
Adhabu hiyo ambayo ni kubwa katika historia ya EPL iliishusha Everton katika msimamo wa ligi hiyo kutoka nafasi ya 14 hadi ya 19 na baada ya kupunguziwa adhabu sasa timu hiyo inapanda kutoka nafasi ya 17 hadi 15.
Everton hata hivyo huenda ikajikuta katika majanga mengine baada ya kushitakiwa mwezi uliopita kwa mara ya pili ikidaiwa kwenda kinyume na kanuni kwa mara nyingine katika misimu mitatu hadi msimu wa 2022-23 na kesi hiyo inatarajia kusikilizwa Aprili 8.
Baada ya kupunguziwa adhabu klabu ya Everton imedai kuridhishwa na uamuzi huo uliotolewa na bodi iliyosikiliza rufaa ya klabu hiyo na ipo tayari kushiriki kikamilifu katika kesi ya pili.
Kupunguzwa kwa adhabu hiyo kunaifanya Everton iwe imejiweka mbali kidogo na janga la kushuka daraja kwa tofauti ya pointi tano bado inalazimika kupambana katika mechi 12 zilizobaki kabla ya msimu huu wa ligi kufikia tamati.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2024/02/26/everton-yapunguziwa-adhabu-epl/feed/ 0
Everton yapokwa pointi 10 EPL https://www.greensports.co.tz/2023/11/18/everton-yapokwa-pointi-10-epl/ https://www.greensports.co.tz/2023/11/18/everton-yapokwa-pointi-10-epl/#respond Sat, 18 Nov 2023 06:49:08 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=8501

London, England
Klabu ya Everton imenyang’anywa pointi 10 katika Ligi Kuu England (EPL) baada ya kukutwa na hatia ya kuvunja kanuni ya ligi hiyo inayohusu faida, adhabu inayoishusha timu hiyo hadi nafasi ya 19.
Adhabu hiyo kubwa katika historia ya EPL inaiweka klabu hiyo mahali pagumu kwani sasa inakuwa imebakiwa na pointi nne tu katika msimamo wa ligi hiyo yenye timu 20.
Mara baada ya kutangazwa adhabu hiyo, Everton walieleza kushtushwa na adhabu waliyoiita kuwa ni kubwa, isiyo na uhalali na ambayo si haki na klabu hiyo inajipanga kuikatia rufaa.
Machi mwaka huu, tume huru ilikabidhiwa jukumu la kushughulikia suala la klabu hiyo na ingawa uamuzi umefikiwa wa kuinyang’anya pointi 10 lakini haikuwekwa wazi kwa undani ni kanuni ipi hasa iliyovunjwa na klabu hiyo.
Everton ilitoa taarifa yake Machi mwaka huu ikieleza kupata hasara kwa mwaka wa tano mfululizo baada ya kuonesha katika taarifa hiyo kuwa ilikuwa na hasara iliyofikia Pauni 4.7 milioni katika mwaka wa fedha wa 2021-22.
Klabu za EPL zinaruhusiwa kuwa na nakisi ya Pauni 105 milioni kwa kipindi cha miaka mitatu na Everton ilikiri kwenda kinyume na kanuni inayohusu faida ya klabu katika kipindi kilichoishia mwaka 2021-22.
Baada ya suala hilo kusikilizwa kwa siku tano tume huru iliyopewa jukumu hilo ilihitimisha kuwa hasara ambayo Everton iliipata katika kipindi hicho ilifikia Pauni 124.5 milioni.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/11/18/everton-yapokwa-pointi-10-epl/feed/ 0
Everton yapona, Leicester yashuka daraja https://www.greensports.co.tz/2023/05/28/everton-yapona-leicester-yashuka-daraja/ https://www.greensports.co.tz/2023/05/28/everton-yapona-leicester-yashuka-daraja/#respond Sun, 28 May 2023 18:22:05 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=6347

London, England
Timu za Leicester na Leeds United zimeungana na Southampton kushuka daraja zikiaga rasmi Ligi Kuu England (EPL) baada ya mechi za leo Jumapili ambazo ni za mwisho huku Everton ikiepuka janga hilo.
Everton ambayo ilikuwa inachungulia kaburi, ushindi wa bao 1-0 ilioupata mbele ya Bournemouth umekuwa na maana kwa timu hiyo ambayo imefikisha pointi 36 ikishika nafasi ya 17 na hivyo kujihakikishia kucheza EPL msimu ujao.
Msimu wa EPL 2022-23 umehitimishwa rasmi kwa mechi za mwisho kuchezwa leo ambapo timu hizo tatu sasa zitacheza Ligi ya Champioship kuanzia msimu ujao wa 2023-24.


Southampton ambayo ilishaaga EPL siku chache zilizopita, imehitimisha mechi yake ya mwisho leo kwa sare ya mabao 4-4 na Liverpool na hivyo kumaliza ligi ikiwa na pointi 25 na ndiyo inayoshika mkia.
Timu ya Leeds ambayo nayo haikuwa katika nafasi nzuri imemaliza ligi ikiwa nafasi ya 18 na pointi 31 na katika mechi ya leo imelala kwa mabao 4-1 mbele ya Tottenham.
Leicester, ambao ni mabingwa wa EPL msimu wa 2015-16, licha ya kupata ushindi wa mabao 2-1 mbele ya West Ham, ushindi huo haukuweza kuwaokoa na janga hilo na wamemaliza ligi wakiwa nafasi ya 19 na pointi zao 34.
Matokeo ya mechi zote za leo ambazo ni za mwisho kwa msimu wa EPL 2022-23 ni kama ifuatavyo…
Arsenal 5-0 Wolves
Aston Villa 2-1 Brighton
Brentford 1-0 Man City
Chelsea 1-1 Newcastle
Crystal Palace 1-1 Nottm Forest
Everton 1-0 Bournemouth
Leeds 1-4 Tottenham
Leicester 2-1 West Ham
Man Utd 2-1 Fulham
Southampton 4-4 Liverpool

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/05/28/everton-yapona-leicester-yashuka-daraja/feed/ 0
Liverpool, Everton matatani https://www.greensports.co.tz/2023/02/17/liverpool-everton-matatani/ https://www.greensports.co.tz/2023/02/17/liverpool-everton-matatani/#respond Fri, 17 Feb 2023 18:32:52 +0000 https://www.greensports.co.tz/?p=5194

Liverpool, England
Klabu mahasimu Liverpool na Everton zimeingia matatani na sasa zinasubiri kuadhibiwa kwa kushindwa kuwazuia wachezaji wao kuingia katika ugomvi katika mechi baina ya timu hizo Jumatatu iliyopita.
Katika mechi hiyo iliyopigwa kwenye dimba la Anfield na Liverpool kutoka na ushindi wa mabao 2-0, katika dakika ya 86 kulitokea mzozo kiasi cha baadhi ya wachezaji kushikana mashati.
Taarifa ya Chama cha Soka England (FA) ilieleza kuwa klabu zote zilishindwa kuwaongoza wachezaji wao katika namna ambayo wangejizuia kufanya matendo yasiyofaa michezoni badala yake hadi wachezaji wa akiba waliingia uwanjani na kuanza kukabiliana.
Andrew Robertson na kipa wa Everton Jordan Pickford walipishana kauli kwa kujibizana baada ya Robertson kuupiga mpira mbali. Wachezaji hao kila mmoja alipewa kadi za njano.
FA imezitaka klabu za Liverpool na Everton ambazo ni mahasimu wa kihistoria, hadi Februari 20 kila moja iwe imejibu hoja hizo.

]]>
https://www.greensports.co.tz/2023/02/17/liverpool-everton-matatani/feed/ 0