Na mwandishi wetu
Klabu ya Azam imeanza kutoa orodha ya wachezaji ambao haitokuwa nao kuelekea msimu ujao na mapema wameanza na mkongwe Daniel Amoah.
Azam imeeleza kuachana na nahodha wake huyo Alhamisi hii baada ya beki huyo raia wa Ghana kudumu ndani ya kikosi hicho kwa misimu nane tangu alipotua mwaka 2017 akitokea Medeama ya nchini kwao.
“Asante kwa utumishi wako wa miaka nane ya nguvu ukiipigania nembo ya klabu yetu, aliyekuwa nahodha wetu, Daniel Amoah, asante kwa kumbukukumbu,” ilieleza taarifa ya Azam kupitia majukwaa yao ya mitandaoni.
Azam ilivutiwa na uwezo wa mchezaji huyo anayemudu nafasi ya beki wa kati na kulia alipokuja na Medeama kuvaana na Yanga kwenye Kombe la Shirikisho Afrika Julai 16, mwaka 2016 katika mchezo ulioisha kwa sare ya bao 1-1.
Baada ya kumaliza msimu wa 2022-23, Amoah aliongeza mkataba wa miaka miwili uliokuwa uishe mwaka 2025 lakini mambo yamekuwa tofauti huku taarifa zaidi zikidai nyota huyo ataendelea kuonekana katika Ligi Kuu NBC baada ya Simba SC kuonesha nia ya kuhitaji huduma yake.
Soka Azam yaachana na Amoah
Azam yaachana na Amoah
Read also